Psalms 65

Kusifu Na Kushukuru

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.

1 aEe Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
2 bEwe usikiaye maombi,
kwako wewe watu wote watakuja.
3 cTulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.
4 dHeri wale uliowachagua
na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako!
Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako,
mema ya Hekalu lako takatifu.

5 eUnatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki,
Ee Mungu Mwokozi wetu,
tumaini la miisho yote ya duniani
na la bahari zilizo mbali sana,
6 fuliyeumba milima kwa uwezo wako,
ukiwa umejivika nguvu,
7 guliyenyamazisha dhoruba za bahari,
ngurumo za mawimbi yake,
na ghasia za mataifa.
8 hWale wanaoishi mbali sana
wanaogopa maajabu yako,
kule asubuhi ipambazukiapo
na kule jioni inakofifilia
umeziita nyimbo za furaha.

9 iWaitunza nchi na kuinyeshea,
waitajirisha kwa wingi.
Vijito vya Mungu vimejaa maji
ili kuwapa watu nafaka,
kwa maana wewe umeviamuru.
10 jUmeilowesha mifereji yake
na kusawazisha kingo zake;
umeilainisha kwa manyunyu
na kuibariki mimea yake.
11 kUmeuvika mwaka taji ya baraka,
magari yako yanafurika kwa wingi.
12 lMbuga za majani za jangwani umezineemesha;
vilima vimevikwa furaha.
13 mPenye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama,
na mabonde yamepambwa kwa mavuno;
vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.
Copyright information for SwhNEN